E-UTALII CONFERENCE
E- Utalii Conference. Its the eTourism & eMarketing Conference to revolutionize Tanzania Tourism Industry for Tanzanian Travel & Tours agency, Tour Guide & Hotel Read more: http://www.e-utaliiconference.com/
WABONGO UGHAIBUNI
TANZANIANS ABROAD NI MTANDAO UNAOKULETEA HABARI,MATANGAZO NA MATUKIO MBALIMBALI KUHUSU WATANZANIA UGHAIBUNI.
Popular Posts
-
Umati wa watanzania waishio nchini Italia jana mchana 14 Jan. 2012, walijumuika kwa pamoja mjini napoli kuuaga mwili wa marehemu ...
-
Sensei Rumadha Fundi maarufu kwa jina la SENSEI ROMI. Kwa kweli ni jambno la kufurahisha na kujivuni sana kuwa Tanzania tunao watu amba...
-
Baadhi ya Watanzania pichani wakisubiri kumsalia marehemu Kwa uwezo wa Allah na ushirikiano wa hali ya juu uliopo kati yetu (watanzania wa ...
-
Jumuiya ya watanzania ugiriki ilisherehekea miaka 48 ya mapinduzi ya Zanzibar kwenye ofisi ya jumuiya J'mosi 14/02.Tulilazimika ...
-
sensei pichani baada ya ushindi wa mpambanaji wake Sensei katika kujinyoosha kabla ya kuanza kufundisha moja ya matukio huko nyuma sensei a...
Thursday, May 17, 2012
Monday, April 30, 2012
Musician Recaptures Tanzanians Lost Glory

Friday, April 27, 2012
Kamati ya muda iliyoteuliwa Ubalozini kwa nia ya kuanzisha chama cha watanzania Sweden inawakaribisha katika hafla fupi yaufunguzi wa chama na pia kuchagua viongozi watakaondeleza shuguli za chama.
Mgeni wa heshima katika ufunguzi na uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Watanzania atakuwa Mh. Balozi Muhammed Mwinyi Haji Mzale.
Sehemu: Tanzania house, Näsby Allè 6, Täby
Atakayependa kugombea uongozi ajaze fomu ya kujiandikisha kugombea uongozi wa chama na kuituma kwa katibu kwa anuani pepe kama inavyoonekana hapo chini.
Thursday, April 26, 2012
MUUNGANO NA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI
Napokea salam zenu za BIRTHDAY kwa niaba ya watanzania wa Ugiriki tulioweza kuungana na kuendelea kuwa pamoja katika mazingira magumu yanayoendelea kutuzunguka.
Tarehe yetu hii ya kuzaliwa 26/04/1964 ni ya kubuni ,tunaitumia kuonesha umuhimu wa ushirikiano na muungano. Ilitakiwa birthday yetu iwe ile siku tuliyoisajili rasmi Jumuiya yetu katika Mahakama ya Mwanzo ya Athens(J’tatu 16/09/2002)
Kwa sisi watanzania tunaoishi Ugiriki,neno “MUUNGANO” hatulitumii katika ile maana ya kisiasa inayotambulika na wengi,na ndiyo maana katika maisha yetu ya kila siku hatuna UDINI, UKABILA WALA(…….)
Hali hii ya MUUNGANO tumeikuta tangu miaka mingi ya nyuma toka kwa wenzetu waliotutangulia. Miaka ya nyuma wengi walioishi nchi hii walikuwa si wakaazi walioamua kujenga familia kama ilivyo sasa.Kumbukumbu zetu zinaonesha mtoto wa kwanza kuzaliwa nchi hii akiwa na baba na mama wote raia wa Tanzania alizaliwa 12/01/1994!!!!( Siku hiyo ni siku ya MAPINDUZI)
Kwa sisi watanzania wa Ugiriki maneno “Muungano” na “Mapinduzi” yanajikuta moja kwa moja yana maana inayotusukuma katika “KUSHIRIKIANA.” Na huu ushirikiano hauna maana kwamba sisi hatuna kasoro la hasha.Hakuna jamii yoyote duniani iliyokamilika.
Tunapenda kuwashukuru wale wote wanaoendelea kuuendeleza “MUUNGANO” wetu.Na tunawashukuru kwa dhati marafiki zetu wote waliojiunga nasi @ fb.
Tunamuomba Mola atupe afya na uzima na atuepushe na mabalaa. (Amen)
KAYU LIGOPORA
KATIBU WA JUMUIYA
Tuesday, April 10, 2012
RAMBIRAMBI KWA FAMILIA YA STEVEN KANUMBA NA WATANZANIA KWA UJUMLA
Sunday, April 8, 2012
Monday, March 12, 2012
UFAFANUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI
UFAFANUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI KUHUSIANA NA “KILIO CHA WATANZANIA UGIRIKI”
Kuna Mdau wa ugiriki aliandika katika blog ya Michuzi 12/03/2012 ‘Kilio cha watanzania ugiriki” na kulikuwa na maoni tofauti yasiyopungua 25.
Kwanza kabla ya yote kichwa chake cha habari kingependeza kiwe “KILIO CHA MTANZANIA” na siyo “KILIO CHA WATANZANIA”
Pili ,kwa kuwa mtandao umeleta usawa wa mtu au watu kueleza chochote wakitakacho,imekuwa ni ada kwa baadhi ya watu kuelezea fikra zao kwa kutumia ANONYMOYS na wengine wakidai wapo nchi fulani kumbe hawapo kabisa katika nchi hiyo.
Mimi niandikae maelezo haya naitwa KAYU LIGOPORA mkaazi wa Athens ni Katibu wa Jumuiya ya watanzania tuliopo hapa. Napatikana kirahisi kwa email tanzathens@yahoo.com.
Nimelazimika kuuandika ufafanuzi huu baada ya kuombwa na watanzania wengi wanaoishi hapa waliosoma “KILIO CHA WATANZANIA UGIRIKI”
Ni kweli kuna hali ngumu ya kiuchumi ugiriki ukilinganisha na ilivyokuwa zamani.Yeyote ataepinga hali hili hatokuwa mkweli wa maelezo(Na huu ni ukweli pekee katika maelezo ya kilio cha Mdau wa Ugiriki).Isipokuwa mdau aliyeelezea kilio chake ametumia maelezo mengi yasiyokuwa na ukweli ili aweze kuwakinaisha wasomaji wakubaliane na hoja zake.
Kwa mfano
1. Anadai kuna majina ya wageni zaidi ya milioni waliojiandikisha kurudi (akiwemo na yeye) .. Hakuna ukweli wa idadi hiyo kulingana na takwimu za idara husika za hapa.
2. Anadai pa kulala wanashindwa kulipa hadi kuna wengine wanajipeleka hospitali ili walazwe wapate pa kulala!!!! Namnukuu “Imebidi baadhi yetu kuna ambao wamejipatisha vitanda hospitalini ili kuweza angalau kupata sehemu ya kuweka ubavu na chakula”…Hapa sina comment nawaachia wasomaji, ila tu nchi hii huwezi KUJIPATISHA KITANDA HOSPITALI KAMA HUUMWI na hasa ukiwa mgeni!!!
Inakuwa vigumu mno kuwakinaisha wasomaji wenye busara zao kwamba watanzania wa ugiriki kilio chao ni hicho kilichoelezwa na Mdau ANONYMOYS wakati kwamba juzi juzi watanzania haohao walikuwa wanajirusha na KHADIJA KOPA NA MATONYA na wanajiandaa kumleta mwimbaji mwingine katika kipindi cha Pasaka!!!!
Mwisho,inabidi wanaokuja Ughaibuni kutafuta maisha waelewe kuwa katika kutafuta kuna tabu tofauti ambazo zitawakumba na wanabidi wazivumilie. Ingekuwa maisha ni rahisi kama wanavyodhani basi kila mmoja angekuja Ughaibuni na kurudi Afrika akiwa milionea.
KAYU LIGOPORA
KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI
Wednesday, February 29, 2012
GREECE:MWILI WA MAREHEMU JAMHURI TUMEUSAFIRISHA LEO.
Pamoja na hali ngumu inayoendelea kutukabili watanzania tunaoishi ugiriki ugumu huo hau...kuweza kutuzuwia kutekeleza ada na mazowea ya kumsafirisha mtanzania yeyote anaefariki hapa.
Jumuiya ya watanzania ugiriki, inawashukuru wale wote walioshiriki kwa hali na mali katika kumsafirisha mwenzetu.
Tunapenda kutoa shukurani maalum kwa Kaimu Balozi wetu Rome Italy kwa kututumia haraka mno "barua ya uthibitisho" iliyoturahisishia kwa kiasi kikubwa harakati zote za kumsafirisha Marehemu.
Tunamuomba Allah amlaze Marehemu mahala pema peponi.(Amin)
INNA LILLAH WAINNA ILAIH RAAJIUUN
Kayu LigoporaKatibu Mkuu
Jumuiya ya watanzania ugiriki
Monday, February 27, 2012
Katibu Mkuu akanusha habari potoshi kuhusu Balozi zetu Nje
Sunday, February 26, 2012
Mkutano wa Jumuiya ya Watanzania Rome wapendeza Kuliko!!
Katibu akiwa pamoja na Yakubu.
Katibu akiwa pamoja na wajume.
Tuesday, February 21, 2012
TMTV:TANGAZO

TUNAWAAHIDI MAMBO MAZURI YANAKUJA,VIDEO KIBAO MPYA ZITAONGEZEKA KWA RAHA ZAIDI KAMA KAWAIDA 24/7 NON-STOP.
Saturday, February 11, 2012
TANGAZO:MKUTANO WA UCHAGUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA ROME

Kwa maelezo zaidi mnakaribishwa kutembelea official Blog ya Jumuiya hapa www.watanzania-roma.blogspot.com.
Monday, January 23, 2012
The Northern League in the parade with the flags of Tanzania:''Give us back the money''
Sunday, January 22, 2012
WATANZANIA SIKU WALIYOMUAGA MAREHEMU TWAHIR HUSSEN OMAR MJINI NAPOLI
![]() |
| Baadhi ya Watanzania waliotoka miji ya mbali na Napoli. |
![]() |
| Pichani alieinamia meza ni Ramadhan Mavumbi akiwa katika majonzi baada ya kusoma wasifu wa marehemu Twahir. |
![]() |
| Baadhi ya Watanzania waliotoka miji ya Modena ,Bologna ,Genova na sehemu zingine |
![]() |
| Pichani kama unakumbukumbu nzuri ya kandanda utawakumbuka hawa wacheza wa enzi izo mzee Waswa na Kassa Mussa. |
![]() |
| Wakina dada pichani wakitoa huduma ya chakula huku wakiwa na tshirt zenye picha ya marehemu Twahir |
Sunday, January 15, 2012
MIAKA 48 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR.. UGIRIKI




























