Popular Posts

Monday, April 30, 2012

Musician Recaptures Tanzanians Lost Glory



Tanzania has regained its lost glory in world of music fame that has dwindled since the eighties.
When the name of Tanzania is currently mentioned in international music circles the name of Ebrahim Makunja popularly known as Ras Makunja of FFU and his “The Ngoma Africa Band” aka FFU based in Germany cannot be slighted. FFU has earnestly strived to place Tanzania in the international music charts.
It is the only Tanzanian band that is based overseas. Its contribution in the music industry both in Tanzania, East Africa and abroad is superb. The band has often been able to bring its records to radio stations back at home.
Many of their hits touch the souls of their fans. Two of their hits, which are very popular in local radio stations and contained in “50 Uhuru Anniversary” CD are “Shangwe”, and “Miaka 50 ya Uhuru”. The rumba style songs are composed by band leader Ras Makunja.
He pairs in singing with the comical solo guitarist Chris-B. Apart from the well composed lyrics and the highly perfected musical beat the songs carry very strong and emotional messages to the community. Their messages are acclaimed not only in Tanzania but world all over.
Ras Makunja of FU, is not only a seasoned tactful and artistic composed. He too has visionary messages to the society. To call him Kamanda (Commander) Ras Makunja is not demeaning him.
He ensured that two of his CDs including “Jakaya Kikwete 2010″ which claimed global fame reached more than 310 radio stations in the world. This CD earned him the mark of being a hard headed musician from some quarters.
His band now dubbed FFU (Fanya Fujo Uone) literally means creates chaos and see, immediately came up with a CD “Anti Corruption Squad” which has the song “Rushwa ni Adui wa Haki”. The fans see this song as the Al-Albadir of the corrupt.
The song was a smash hit within Tanzanians. It placed Ras Makunja and his band ‘Ngoma Afrika’ not only as ordinary musicians in the musical arena. They had something else to offer the society apart from the usual entertainment. Visionary eye opening and soul searching messages.
Yet despite all this no one seems to realize the onerous task that this musicians does. They have never been ordained with a single medal here at home. As a popular Swahili goes “Asiyekuwepo na lake halipo” (He who is not there (present) so is his/her share). Ras Makunja and Ngoma Afrika may not be with us, but his works and messages are!
The official web of the band is http://www.ngoma-africa.com/ One can become a fan member of the band by signing up. The good work the band is doing in promoting Tanzania in the field of music deserves local support both in cash and form.








Friday, April 27, 2012

CHAMA CHA WATANZANIA SWEDEN

(TANZANISKA RIKSFÖRBUNDET)
Kwa watanzania pamoja na marafiki!

Kamati ya muda iliyoteuliwa Ubalozini kwa nia ya kuanzisha chama cha watanzania Sweden inawakaribisha katika hafla fupi yaufunguzi wa chama na pia kuchagua viongozi watakaondeleza shuguli za chama.

Mgeni wa heshima katika ufunguzi na uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Watanzania atakuwa Mh. Balozi Muhammed Mwinyi Haji Mzale.

Sehemu: Tanzania house, Näsby Allè 6, Täby

Tarehe na Wakati: Tarehe 28 Aprili 2012: Saa tisa mchana mpaka saa kumi na moja jioni (saa 9 mchana - 11 Jioni).

Atakayependa kugombea uongozi ajaze fomu ya kujiandikisha kugombea uongozi wa chama na kuituma kwa katibu kwa anuani pepe kama inavyoonekana hapo chini.


Wote mnakaribishwa na ukipata taarifa hii tafadhali mtumie na mwingine!

Kamati ya wanamchakato kupitia

Katibu wa Muda

Bi. Angela Wilberd:


Thursday, April 26, 2012

MUUNGANO NA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI

Napokea salam zenu za BIRTHDAY kwa niaba ya watanzania wa Ugiriki tulioweza kuungana na kuendelea kuwa pamoja katika mazingira magumu yanayoendelea kutuzunguka.

Tarehe yetu hii ya kuzaliwa 26/04/1964 ni ya kubuni ,tunaitumia kuonesha umuhimu wa ushirikiano na muungano. Ilitakiwa birthday yetu iwe ile siku tuliyoisajili rasmi Jumuiya yetu katika Mahakama ya Mwanzo ya Athens(J’tatu 16/09/2002)

Kwa sisi watanzania tunaoishi Ugiriki,neno “MUUNGANO” hatulitumii katika ile maana ya kisiasa inayotambulika na wengi,na ndiyo maana katika maisha yetu ya kila siku hatuna UDINI, UKABILA WALA(…….)

Hali hii ya MUUNGANO tumeikuta tangu miaka mingi ya nyuma toka kwa wenzetu waliotutangulia. Miaka ya nyuma wengi walioishi nchi hii walikuwa si wakaazi walioamua kujenga familia kama ilivyo sasa.Kumbukumbu zetu zinaonesha mtoto wa kwanza kuzaliwa nchi hii akiwa na baba na mama wote raia wa Tanzania alizaliwa 12/01/1994!!!!( Siku hiyo ni siku ya MAPINDUZI)

Kwa sisi watanzania wa Ugiriki maneno “Muungano” na “Mapinduzi” yanajikuta moja kwa moja yana maana inayotusukuma katika “KUSHIRIKIANA.” Na huu ushirikiano hauna maana kwamba sisi hatuna kasoro la hasha.Hakuna jamii yoyote duniani iliyokamilika.

Tunapenda kuwashukuru wale wote wanaoendelea kuuendeleza “MUUNGANO” wetu.Na tunawashukuru kwa dhati marafiki zetu wote waliojiunga nasi @ fb.

Tunamuomba Mola atupe afya na uzima na atuepushe na mabalaa. (Amen)

KAYU LIGOPORA

KATIBU WA JUMUIYA

Tuesday, April 10, 2012

RAMBIRAMBI KWA FAMILIA YA STEVEN KANUMBA NA WATANZANIA KWA UJUMLA



            Steven Kanumba


TMTV a.k.a TANZANIA MUSIC TELEVISION INATOA RAMBIRAMBI ZAKE KWA FAMILIA YA MSANII WA FILAMU STEVEN KANUMBA
NA WATANZANIA WOTE KWA UJUMLA KWA MSIBA MKUBWA ULIOTUKUTA.KIFO CHA STEVEN KANUMBA KIMEWAGUSA WASANII
WOTE WA FANI MBALIMMBALI NA WATANZANIA WOTE KWA UJUMLA.
TUNAOMBA KWA PAMOJA MWENYEZI MUNGU AILAZE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YA MWENZETU STEVEN KANUMBA
AMEEN.

TMTV
UTAWALA.

Monday, March 12, 2012

UFAFANUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI

UFAFANUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI KUHUSIANA NA “KILIO CHA WATANZANIA UGIRIKI”

Kuna Mdau wa ugiriki aliandika katika blog ya Michuzi 12/03/2012 ‘Kilio cha watanzania ugiriki” na kulikuwa na maoni tofauti yasiyopungua 25.

Kwanza kabla ya yote kichwa chake cha habari kingependeza kiwe “KILIO CHA MTANZANIA” na siyo “KILIO CHA WATANZANIA”

Pili ,kwa kuwa mtandao umeleta usawa wa mtu au watu kueleza chochote wakitakacho,imekuwa ni ada kwa baadhi ya watu kuelezea fikra zao kwa kutumia ANONYMOYS na wengine wakidai wapo nchi fulani kumbe hawapo kabisa katika nchi hiyo.

Mimi niandikae maelezo haya naitwa KAYU LIGOPORA mkaazi wa Athens ni Katibu wa Jumuiya ya watanzania tuliopo hapa. Napatikana kirahisi kwa email tanzathens@yahoo.com.

Nimelazimika kuuandika ufafanuzi huu baada ya kuombwa na watanzania wengi wanaoishi hapa waliosoma “KILIO CHA WATANZANIA UGIRIKI”

Ni kweli kuna hali ngumu ya kiuchumi ugiriki ukilinganisha na ilivyokuwa zamani.Yeyote ataepinga hali hili hatokuwa mkweli wa maelezo(Na huu ni ukweli pekee katika maelezo ya kilio cha Mdau wa Ugiriki).Isipokuwa mdau aliyeelezea kilio chake ametumia maelezo mengi yasiyokuwa na ukweli ili aweze kuwakinaisha wasomaji wakubaliane na hoja zake.

Kwa mfano

1. Anadai kuna majina ya wageni zaidi ya milioni waliojiandikisha kurudi (akiwemo na yeye) .. Hakuna ukweli wa idadi hiyo kulingana na takwimu za idara husika za hapa.

2. Anadai pa kulala wanashindwa kulipa hadi kuna wengine wanajipeleka hospitali ili walazwe wapate pa kulala!!!! Namnukuu “Imebidi baadhi yetu kuna ambao wamejipatisha vitanda hospitalini ili kuweza angalau kupata sehemu ya kuweka ubavu na chakula”…Hapa sina comment nawaachia wasomaji, ila tu nchi hii huwezi KUJIPATISHA KITANDA HOSPITALI KAMA HUUMWI na hasa ukiwa mgeni!!!

Inakuwa vigumu mno kuwakinaisha wasomaji wenye busara zao kwamba watanzania wa ugiriki kilio chao ni hicho kilichoelezwa na Mdau ANONYMOYS wakati kwamba juzi juzi watanzania haohao walikuwa wanajirusha na KHADIJA KOPA NA MATONYA na wanajiandaa kumleta mwimbaji mwingine katika kipindi cha Pasaka!!!!

Mwisho,inabidi wanaokuja Ughaibuni kutafuta maisha waelewe kuwa katika kutafuta kuna tabu tofauti ambazo zitawakumba na wanabidi wazivumilie. Ingekuwa maisha ni rahisi kama wanavyodhani basi kila mmoja angekuja Ughaibuni na kurudi Afrika akiwa milionea.

KAYU LIGOPORA

KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI

Wednesday, February 29, 2012

GREECE:MWILI WA MAREHEMU JAMHURI TUMEUSAFIRISHA LEO.

Kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu na jitihada zetu tumefanikiwa kumsafirisha marehemu HAROUN ABDALLAH OTHMAN (Maarufu kwa jina la JAMHURI) ili akazikwe nyumbani.Mwili wa Marehemu utawasili Dar Alhamisi 01/03 saa nane na nusu usiku kwa ndege ya Turkish airline (TK603)

Pamoja na hali ngumu inayoendelea kutukabili watanzania tunaoishi ugiriki ugumu huo hau...kuweza kutuzuwia kutekeleza ada na mazowea ya kumsafirisha mtanzania yeyote anaefariki hapa.

Jumuiya ya watanzania ugiriki, inawashukuru wale wote walioshiriki kwa hali na mali katika kumsafirisha mwenzetu.

Tunapenda kutoa shukurani maalum kwa Kaimu Balozi wetu Rome Italy kwa kututumia haraka mno "barua ya uthibitisho" iliyoturahisishia kwa kiasi kikubwa harakati zote za kumsafirisha Marehemu.
Tunamuomba Allah amlaze Marehemu mahala pema peponi.(Amin)

INNA LILLAH WAINNA ILAIH RAAJIUUN

Kayu LigoporaKatibu Mkuu
Jumuiya ya watanzania ugiriki

Monday, February 27, 2012

Katibu Mkuu akanusha habari potoshi kuhusu Balozi zetu Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule (katikati), akikanusha na kurekebisha taarifa potoshi zilizoandikwa katika baadhi ya magazeti kuhusu Mabalozi na watumishi wake nje ya nchi.  Pichani ni Bw. Lupakisyo Mwakitalima (Kulia), Mhasibu Mkuu Wizarani na Bw. Assah Mwambene (kushoto), Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Sunday, February 26, 2012

Mkutano wa Jumuiya ya Watanzania Rome wapendeza Kuliko!!

Kama ilivyokuwa imepangwa, jana tarehe 25 Feb. 2012 kwenye ukumbi wa Ubalozi wa Tanzania Italy, mjini Rome, ulifanyika mkutano wa Jumuiya ya Watanzania Roma. Mkutano huu ambao ulikuwa uambatane na uchaguzi wa viongozi wapya ulifana sana japo wanajumuiya hai hawakuwa zaidi ya nusu ya Wanajumuiya wote. Kutokana na kutokuwepo kwa wanajumuiya zaidi ya nusu, wanajumuiya kwa pamoja waliamua kuupeleka uchaguzi mbele mpaka mwishoni mwa mwezi wa nne, ili kuweza kuandaa mazingira mapya yatakayo fanikisha zoezi ili la uchaguzi. Mgeni wa heshima kwenye mkutano huu alikuwepo Kaimu Balozi wa ubalozi wa Tanzania nchini Italy mh. Salvatory Mbilinyi. Kwenye huu mkutano, wanajumuiya kwa Pamoja walijadili maswala mbalimbali ya kujenga jumuiya kama vile, umuhimu wa kushiriki kwenye vikao mbalimbali vya jumuiya, kujitaidi kutoa michango ya jumuiya na mengineyo mengi. Siku chache zijazo, Kamati ya Utendaji ya jumuiya ya Watanzania Rome, itakaa ili kujadili maandalizi ya sherehe ya muungano wa Tanzania itakayofanyika mwishoni mwa mwezi wa nne. Mara tu kamati ya utendaji itakapo kaa mtajulishwa hatua itakayo fuata.
Hapa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Rome, Mh. Leonce Uwandameno (aliyesimama) akifungua mkutano. Kushoto ni Katibu wa Jumuiya Andrew Chole Mhella na kulia ni Mweka Hazina ndugu Awadhi Suleiman.



Hapa uongozi wa Jumuiya ukimkabidhi Bi.Gunhild Mwakangale kadi tatu za uanajumuiya. Kadi mbili zingine atazifikisha kwa Bi. Alice Maimu na Bi. Hadija Omari Mwakangale. Hawa wote wanaishi Sardegna kusini kwa Italy.
Wajumbe wakilisakata KWAITO.
Kama mnavyoona, wajumbe wakiandaa kitu tumbo yapenda.
Mwenyekiti akipata picha ya pamoja na Wanajumuiya.
Hapa Bi Gunhild akisho some love kwa Mjumbe, Bi. Thanner.
Katibu akiwa pamoja na Yakubu.
Katibu akiwa pamoja na wajume.

Tuesday, February 21, 2012

TMTV:TANGAZO


WAPENDWA WATAZAMAJI WA TMTV.
TUNAPENDA KUWATANGAZIA KUWA KUTOKANA NA MATATIZO YA KIUFUNDI.
KUMEKUWA NA TATIZO LA KUINGIA KTK TV KATIKA SIKU CHACHE ZILIZOPITA.TATIZO HILO LINAENDELEA KUFANYIWA KAZI.
KWA SASA UNAWEZAENDELEA KUBURUDIKA NA TMTV KWA LINK HII  http://tmtv.eightzerodigital.com/player.php

TUNAWAAHIDI MAMBO MAZURI YANAKUJA,VIDEO KIBAO MPYA ZITAONGEZEKA KWA RAHA ZAIDI KAMA KAWAIDA 24/7 NON-STOP.


Saturday, February 11, 2012

TANGAZO:MKUTANO WA UCHAGUZI WA JUMUIYA YA WATANZANIA ROME


Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Rome, unayofuraha kuwajulisheni kuwa siku ya jumamosi tarehe 25 februari 2012 kuanzia saa nane mchana, kutakuwa na mkutano wa uchaguzi wa viongozi wapya wa Jumuiya ya Watanzania Rome. Mkutano huu utafanyika kwenye ukumbi wa ubalozi wa Tanzania Italy, mjini Rome uliopo kwenye mtaa wa Via Cortina d'ampezzo 185. Wanajumuiya hai wote mnaombwa muwasiliane na katibu ndugu Andrew Chole Mhella ili muweze kupata taratibu nzima za Mkutano huu. Mnaweza kumpata katibu kwa e-mail hii watanzaniaroma@yahoo.it. au kwa simu namba 3479094800. Kwa wale ambao wanapenda kuwasilisha majina yao kwaajiri ya kugombea nafasi hizi mnaombwa mtume majina yenu yakiambatanishwa na nafasi ambayo mnataka kugombea kupitia e-mail ya jumuiya hapo juu. Nafasi ni hizi MWENYEKITI, MWENYEKITI MSAIDIZI, KATIBU, KATIBU MSAIDIZI, MWEHA HAZINA NA NAFASI MBILI ZA WAJUMBE.

Kwa maelezo zaidi mnakaribishwa kutembelea official Blog ya Jumuiya hapa www.watanzania-roma.blogspot.com.

Monday, January 23, 2012

The Northern League in the parade with the flags of Tanzania:''Give us back the money''



I leghisti in corteo con le bandiere della Tanzania: ''Ridateci i soldi''
Tra i motivi della rabbia della base leghista esplosa durante la manifestazione di Milano, anche le notizie dei recenti investimenti del partito in Tanzania. E così un folto gruppo di manifestanti ha deciso di protestare portando in spalla le bandiere dello stato africano. "Quei soldi sono delle sezioni, li rivogliamo indietro", dicono (video di Marco Billeci)

Among the reasons for the anger of the League based in Milan exploded during the event, even the news of the party's recent investments in Tanzania. And so a large group of protesters decided to protest over his shoulder carrying the flags of the African state. "That money are sections of them I want them back," says (Mark Billeci video)
video

Sunday, January 22, 2012

NY: MZEE YUSUF NDANI YA BIG APPLE


Mzee Yusuf akutana na Washabiki Big Apple!

WATANZANIA SIKU WALIYOMUAGA MAREHEMU TWAHIR HUSSEN OMAR MJINI NAPOLI

Baadhi ya Watanzania waliotoka miji ya mbali na Napoli.

Pichani alieinamia meza ni Ramadhan Mavumbi  akiwa katika majonzi baada ya kusoma wasifu wa marehemu Twahir.

Baadhi ya Watanzania waliotoka mji mkuu Roma ,pichani ni Katibu wa jumuiya ya Watanzania Roma ndugu Andrew Mhella , katikati ni Ofisa wa ubalozi na mweka hazina wa jumuiya ya watanzania Roma ndugu Awadh.

Baadhi ya Watanzania waliotoka miji ya Modena ,Bologna ,Genova na sehemu zingine
,

Pichani kama unakumbukumbu nzuri ya kandanda  utawakumbuka hawa wacheza wa enzi izo  mzee Waswa na Kassa Mussa.

Wakina dada pichani wakitoa huduma ya chakula huku wakiwa na tshirt zenye picha ya marehemu Twahir

Picha na George Mayaka
Copyright © 2012  George Mayaka  All rights reserved.
Kwa picha zaidi Gonga hapa GEORGE MAYAKA.

Sunday, January 15, 2012

MIAKA 48 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR.. UGIRIKI











Jumuiya ya watanzania ugiriki ilisherehekea miaka 48 ya mapinduzi ya Zanzibar kwenye ofisi ya jumuiya J'mosi 14/02.Tulilazimika kuichelewesha kwa siku mbili kutokana na mihangaiko ya kikazi.

Sherehe zilianza kwa wimbo wa Taifa na kufuatiwa na risala fupi ya Mwenyekiti mwanzilishi wa Jumuiya yetu bw.Suleiman Nassib (DIDOS)ambae alisisitizia umuhimu wa umoja na ushirikiano.

Ilifuatiwa na shukurani za bi.Joan mwakilishi wa kikundi cha wanafunzi wa Holland tuliowakaribisha rasmi katika sherehe yetu.

Baadae mke wa Mwenyekiti Bi Asha Chunda alikata keki maalum ya mapinduzi na bw.Jackson na bi Sandra walitumbuiza na kuchangamsha ukumbi kwa nyimbo zao zilizowanyanyua hata wageni wetu.

Sherehe ziliendelea hadi alfajiri

KAYU LIGOPORA

KATIBU WA JUMUIYA YA WATANZANIA UGIRIKI



UMATI WA WATANZANIA NCHINI ITALY WAUAGA MWILI WA MAREHEMU TWAHIR HUSSEIN OMARI MJINI NAPOLI







Umati wa watanzania waishio nchini Italia jana mchana 14 Jan. 2012, walijumuika kwa pamoja mjini napoli kuuaga mwili wa marehemu Twahir Hussein Omari, maarufu kwa wengi kwa jina la utani la "Mboga Zote". Mwili wa marehemu utasafirishwa siku ya Jumanne tokea Rome Fiumicino airport kuelekea Dar-es-salaam na shirika la ndege la KLM na kisha kupelekwa mkoani Tanga kwa mazishi.Mwenyezi Mungu mlaze marehemu mahala pema peponi amen.Picha zaidi zitafuata muda si mrefu.