Ticker

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

TUANZIE WAPI?



 TUANZIE WAPI?

Lengo kuu la maandishi yangu siyo kutaka kubadilisha mambo,bali napenda kusikiliza rai tofauti  na marekebisho toka kwa ndugu na marafiki wataosoma uchambuzi wangu ambao ulikuwa umenikaa kooni muda mrefu na nilikuwa natafuta nafasi ya kuumwaga hadharani kwa wenzangu wenye mtazamo mzuri zaidi waweze kunisahihisha ili nami nizinduke.
Baada ya kuangalia kwa utulivu jinsi maamuzi na mabadiliko yanavyofikiwa katika nchi zetu za kiafrika na sehemu nyingi duniani , nimefikia kukinaika ,kuna makundi matatu makuu yanayotuongoza au yanayotusukuma kufikia maamuzi fulani. Na kila kundi lina sifa na nguvu za kuathiri zinazotofautiana na kundi jingine. SIZUNGUMZII INDIVIDUALS WALIOMO NDANI YA MAKUNDI HAYO BALI NAZUNGUMZIA MAKUNDI AS MECHANISM.
Kundi la kwanza :WANASIASA
Kundi la pili:MATAJIRI WAKUBWA(Siyo wajasiriamali wala wanauchumi)
Kundi la tatu: VIONGOZI WA DINI. Siyo dini ni “VIONGOZI WA DINI” yoyote anayoiamini kila mmoja wetu.
Kila kundi lina sifa na mfumo tofauti na jingine . Kati ya kundi  la kwanza na la pili kuna kijikundi kina nguvu za ajabu, kikundi hiki ni cha “USALAMA NA UPELELEZI”. Aidha kuna kijikundi kingine cha WACHUNGA MASLAHI”. Wahusika wa kikundi hiki hujihusisha na kujiingiza katika makundi yote matatu kulingana na hali ya maslahi itavyowavuta. Kijikundi hiki ni hatari mno, hakina simile katika kuhakikisha wanafanikisha kile wakitakacho au kile walichotakiwa wakifanye ili mradi lengo likamilike.Tofauti muhimu iliyopo kati ya kijikundi hiki na wale MATAJIRI WAKUBWA ni kuwa wahusika wa kijikundi hiki HUJIFICHA  na huonekana tu matunda ya vitendo vyao.Wachache hujulikana baada ya mibiginyo inayofanywa ili pia kulinda maslahi makuu.
NB. Sikutaja kundi la WANAJESHI ambao kila demokrasia inavyozidi kukua Afrika wanajikuta ni kundi la kutekeleza maamuzi ya wanasiasa - hata kama hawakubaliani nayo-(WITH EXCEPTION OF EGYPT RECENTLY) tofauti na miaka ya nyuma  walipokuwa wakifanya mapinduzi ya mara kwa mara. Aidha sikutaja vyombo vya habari ambavyo vyote vipo chini ya MATAJIRI WAKUBWA au WANASIASA . Ama wale wanaojiita wanablogs wao nawaweka katika kundi la “WACHUNGA MASLAHI” kwani ni wachache mno kati yao wanaoelezea fikra zao huru.
Kundi la kwanza : WANASIASA.
Sifa kuu za kundi hili ni: UONGO NA KUBADILISHA MISIMAMO
Hakuna kiongozi yeyote duniani aliyetekeleza kikamilifu yale yote aliyoyaahidi kabla ya kuchaguliwa kuwa kiongozi.Ajabu ya mambo sisi waongozwa kila siku tunawataka wawe wakweli na wasibadili misimamo!!!Nadhani kuna sababu ya wazi inayowalazimu wajivishe sifa hii, sababu ambayo sisi waongozwa daima haitugusi katika maisha yetu ya kila siku,Sababu hiyo ni kuwa wanapoingia madarakani hukumbana na mibiginyo na facts tofauti zinazowalazimu wabadilishe misimamo yao ili waweze kuendeleza kuwa Viongozi. Mibiginyo hii inamkumba kila kiongozi bila kujali ukubwa na nguvu ya nchi anayoiongoza!!
Kila mmoja anaweza kuihisi hali hii katika nafasi yoyote ya uongozi wa kijamii aliyowahi kuisimamia.


Kundi la pili : MATAJIRI WAKUBWA.
Sifa kuu za kundi hili ni : KUPATA WAKITAKACHO BILA KUJALI NJIA ILIYOTUMIKA
Hawa ni watekelezaji wakuu wa Machiavellism “End justifies the means” . Ukiangalia kwa makini vita na maafa mengi duniani yamechochewa na kundi hili ambalo lina nguvu kubwa  ya kichinichini katika kulilazimisha kundi la kwanza (wanasiasa )ili lichukue maamuzi yatayolingana na matakwa na maslahi yao.
Hili ni kundi pekee ambalo wahusika wake HAWAJIFICHI  katika kuhakikisha wanapata wakitakacho.Misimamo yao ipo wazi mno na wala haina mizunguko.Hawatumii unafiki wa maadili  kama wanavyofanya wahusika wa kundi la kwanza (wanasiasa)na wa kundi la tatu “A” kama tutavyoona hapo mbele.
Kundi la tatu :VIONGOZI WA DINI.
Kundi hili linagawanyika katika sehemu mbili kuu.”A” na “B”.Kundi la .”A”ni lile la wale wanaotumiwa kwa maslahi ya WANASIASA NA MATAJIRI WAKUBWA.Ama kundi la “B”.ni lile la wale wachache wanaojaribu kufuata dini bila kujali maslahi ya kundi la kwanza wala la pili.Mara zote kila mmoja hudai kuwa yumo katika kundi la “B”.Ila huwa si tabu kuwagundua wapi walipo na hasa kama watatakiwa watoe maamuzi yatayopingana na maslahi ya WANASIASA au MATAJIRI WAKUBWA.
Sifa kuu za kundi la tatu “A” ni :KUWALAGHAI WAUMINI.
Wahusika wa kundi hili, ndani ya nyoyo  zao wana misimamo ya kundi la  kwanza na la pili ila wanapokutana na waumini wao hujilazimisha waonekane kama wapo pamoja nao kumbe sivyo!!!
Sifa kuu za kundi la tatu “B” ni: KUJITENGA AU KUTENGWA.
Wahusika wa kundi hili wamejigawa katika sehemu mbili.Ya kwanza ni wale waliokwisha gundua kuwa hawawezi kufikisha mafunzo halisi ya dini zao bila kuingiliwa na makundi makuu niliyokwisha  taja hapo nyuma na matokeo yake huamua KUJITENGA na kutekeleza dini zao bila marumbano.Ama sehemu ya pili ni ile ya wale wanaoendelea kuamini kuwa wana nafasi ya kuweza kufikisha mafunzo halisi kwa waumini wao na huendelea kupambana na makundi makuuu na mara nyingi hufikia KUTENGWA ili wasiharibu maslahi ya wengine!!!

MWISHO nafungia kwa imani ninayoiamini kwa dhati kuwa tumekuja duniani miaka kadhaa iliyopita na kila mmoja ataondoka baada ya miaka kadhaa na kuiwacha dunia ikiendelea kama ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita. Katika kipindi hiki cha miaka kadhaa tunayoishi HATUNA UWEZO WA KUBADILISHA DUNIA BALI tuna uwezo wa kujaribu KUREKEBISHA BAADHI YA MACHACHE YANAYOTUZUNGUKA KATIKA JAMII ZETU.

JE TUANZIE WAPI?

TUANZIE HAPA  (…………..KUANZA KUJITAMBUA NA KUONDOKANA NA FIKRA HASI ZILIZOPANDIKIZWA KATIKA VICHWA VYETU(kwa maslahi ya wachache) KWAMBA SISI WAAFRIKA MUNGU KATUUMBA TUBAKI KATIKA UNYONGE NA UDHALILI  HADI SIKU YA KIYAMA.)TUSITAKE MABADILIKO YA GHAFLA(ambayo hutukatiksha tamaa tunaposhindwa kuyafikia) TUANZE KWA KUREKEBISHA MACHACHE NA KUSIFU KILA JEMA LINALOFANYIKA KATIKA JAMII ZETU.HATA KAMA LITAFANYWA NA TUSIYEMPENDA.

KAYU LIGOPORA
ATHENS – GREECE
27 AUGUST 2013

Post a Comment

0 Comments